Friday 16 August 2013


               Mkate wa nyama ndani

Mahitaji
Unga wa ngano kilo moja
Nyama ya kusaga nusu kilo
Chumvi kijiko kimoja cha chai
Sukari kijiko cha chakula 1
Mayai mawili
Samli vijiko viwili vya viwili/butter
Maziwa kikombe kimoja (mag)
Hamira pakti moja
Backing powder kijiko cha chai 1
Ndimu/limau vijiko vya chakula viwili
Tangawizi kijiko cha chai 1
Kitunguu swaumu kijiko cha chai 1

Jinsi ya kupika
Chemesha nyama yako ya kusaga  weka ndimu,chumvi,tangawizi na vitunguu swaumu hadi Maji ya kauke iache ipoe.

Katika bakuli weka  unga wako tia hamira,backing powder,sukari,pinch ya chumvi
Samli au batter,yai moja,mimina maziwa kanda hadi unga wako ulainike uwe Kama unga wa buns .
Uache kwa muda wa saa moja utamuka katakata matonge makubwa kiasi sukuma duara paka butter halafu weka nyama ya kusaga halafu roll weka katika chombo cha kuokea,ukimaliza kuzifunga zote ziache kwa nusu saa.
Baada ya nusu saa zipake ute wa Yai juu halafu ingiza katika oven weka moto 180 kwa dk 20 hadi 25.

Thursday 8 August 2013

Mahitaji
Biringa nyembamba ndefu
Kitunguu saumu ya kutwanga kijiko 1cha chai
Chumvi kijiko 1 cha chai
Binzari ya manjano kijiko 1 cha chai
Jeera powder kijiko 1 cha chai
Pilipili ya unga(masala)kijiko 1cha chai
Giligilani ya unga kijiko 1cha chai
curry powder kijiko 1 cha chai

Jinsi ya kupika

Osha biringanya zako vizuri zipasue kwa urefu mara mbili,Weka kando. 
Changanya viungo(spice) vyote kisha jaza kwenye hizo biringanyi. 
Zipange kwny sufuria kama inavyoonekana katika picha,
Weka mafuta kidogo,weka jikoni mafuta yakianza kuchemka punguza moto funika ziive kwa mvuke(steam) kisha geuza upande wa pili nao uive.
Acha dakika kumi baada hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.
Biringanya hizi waweza kuzitumia kwa mihogo,ugali,wali,chapati.

                Mahitaji
       Hapo ya kugeuza upande wa pili na          baada ya kugeuza.
         Baada ya kuiva tayari kwa kuliwa

Mie nilitumia kwa pilau
Nitakutakia pishi jema.
Mahitaji
Nyama ya kusaga nusu
Chumvi kijiko cha chai kimoja 
Pilipili mtama nusu kijiko cha chai
Hoho Tatu rangi tofauti tofauti
Mafuta nusu chupa
Mayai 10
Unga wa mkate(crumbs bread)
Manda za sambusa
Vitunguu Maji vikubwa vitatu
Swaumu nusu kijiko cha chai
Korianda kiasi
Tangawizi kijiko cha chai kimoja

Jinsi kupika

Unachukua nyama yako ya kusaga unatia spice zote unazotaka unaibandika jikoni unaicha ichemke hadi iive.
Halafu unakatakata pilipili boga za kijani njano na nyekundu unakata ndogondogo.
Unakataka vitunguu vyako Kama vile vya sambusa unaweka kando.
Unachukua mayai yako unatapiga unaweka kando.

Unaweka chuma cha chapati jikoni unakaanga mayai,unaweka nyama na vitunguu
Ukishakaanga ukitaka kuligeuza Yai ndo unatia zile pilipili boga.


 Kama inavyoonekana katika picha unatumia manda ya sambusa unaweka mbili mbili then unakunja halafu inakatakata vipande vya size.


Kisha unachukua na ule unga wa mkate mkavu.
Halafu unapiga mayai yako unachovya kidude ndani ya mayai halafu hpembeni unazungushia huo unga wa mkate kama unalizungusha hilo gurudumu isiwe Kati huku pembeni halafu unakaanga kwenye mafuta

Tayari kwa kuliwa,hapo nimetengeneza na chatine


Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!