Sunday 24 November 2013



Mahitaji

Unga wa ngano 250g

Butter 250g

Mayai 9

Baking powder kijiko cha chai1

kuku wa kusaga 2cups 

Chumvi kijiko cha chai 1

Sukari 1/3cup

Kungu manga 1/2 kijiko cha chai(sio lazima)

Mdalasini kijiko cha chai 1

Curry powder kijiko cha chai 1

Kitunguu swaumu kijiko cha chai 1

Tangawizi kijiko cha chai 1

Chicken stock kijiko 1/2 cha chai

Pilipili mtama 1/2 kijiko cha chai

Ndimu/limau moja

Pilipili hoho 1/2 kila rangi


Jinsi ya kupika

Muoshe kuku wako vizuri as iwe na ngozi muweke viungo vyote mbandike jikoni isipokuwa usiweke pilipili hoho.

Mwache achemke na hayo Maji yakikauka muweke pembeni apoe.

Kama utakuwa haujapata kuku wa kusaga umechemsha kuku mzima basi akipoa mnyambue nyambue au msage katika blender,muweke pembeni.

 Saga siagi na sukari pamoja na mayai 3,yakichanganyika weka unga na baking powder.

Ikichanganyika vizuri weka katika chombo cha kuchomea,chukua kuku wako  changanya na mayai 3 mimina juu ya ule unga wako wa keki uliopo katika chombo cha kuchomea,halafu piga Yale mayai matatu yaliyobakia ya changanye na pilipili hoho miminia juu.

Weka katika oven moto 350.


0 comments:

Post a Comment

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!