Saturday 30 January 2016

Mahitaji:-
Viazi mbatata kg 1
Cornflour(starch) vijiko 2 chakula 
Siagi vjk 2 chakula
Chumvi kijiko1 chai
Tomato ketchup vijiko 3 chakula
Tomato puree kijiko 1 chakula
Tandoor masala powder 1/2 kjk chai
Kitunguu saumu kilichosagwa 1/4 kijiko chai
Pili pili ya unga (red chili powder) 1/4 kijiko chai
Binzari ya unga( cumin powder) 1/4 kijiko chai
Manjano (turmeric) 1/8 kijikocchai
Pilipili ya kijani ilokatwa katwa ( green chilli) 1
Limao kipande
Mafuta ya kukaangia
Mkono mmoja kotmir kupambia (for garnish)

MAELEKEZO:-
1.Tia mafuta ktk frying pan au sufuria jikoni , moto uwe wa kati (mediuh heat). Kaanga chips zako

2.Epua acha zichuje mafuta katika paper towels kisha utazikaanga tena kwa mara ya pili zikauke zadi

3. Katika sufuria jikoni pasha moto siagi iyeyuke,toa sufuria jikoni kisha tia cornflour,pamoja na mahitaji yote isipokuwa limao na kotmir.

4 Rudisha sufuria jikoni na kisha changanya vitu vyote ukikoroga hadi mchanganyiko uwe mzito.

5 Punguza moto kisha tia chips zako na geuza zienee viungo vizuri

6 Epua kisha kamulia limao na nyunyiza kotmir ulizokata kata juu. Masala chips tayari kwa kula.

Kijiko cha chai (teaspoon)
Kijiko cha chakula (Tablespoon)

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!