Saturday 9 January 2016

Mahitaji

Ndizi Tamu 5
Kikopo kimoja cha Nazi
Chimvi pinch Mbili
Sukari kijiko cha chakula kimono
Iliki kijiko cha chai kimoja
Custard powder kijiko cha chai kimoja
Maziwa wa unga kijiko cha chakula kimoja
Maji  mag moja

Jinsi ya kupika
Katakakata ndizi zako,ndizi moja toa vipande vinne panga katika sufuria,weka  chumvi,sukari,iliki,mimina maji bandika bikini funika maji yakiukia weka nazi yako wacha ichemke usinifike,wacha kwa dk 3,chukua maziwa yako ya unga (nimetumia nido) weka katika kikombe,weka custard powder changanya na maji moto robo kikombe hakikisha vimelainika mimina katika ndizi wacha kwa dakika 3  epua ndizi zako tayari,
Chakula hiki ni  kwa ajili ya watu watatu.
Unaweza kutumia kwa chai,uji wa Dona,sembe,bada/unga wa muhogo.
Nb: ndizi zisiwe zimeiva sanaaa kuepuka kuhorojeka wakati wa kupika.
Enjoy pishi lako.

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!