Sunday 6 September 2015



Mahitaji

Mchele 2 cups(inategemea na familia yako)

Chumvi nusu kijiko cha chai

Korianda vijiko vitatu vya vyakula(majani)

Soya souse vijiko viwili vya chakula

Vitunguu maji vikubwa vitano.



Kitoweo

Kuku 1/nyama kilo moja

Mahitaji

Kitunguu swaumu kijiko cha chakula kimoja

Tangawizi kijiko cha chakula 1

Paprika kijiko cha chakula 1

Pilipili mtama 1kijiko cha chai

Pilipili mbuzi iliyosagwa 1/2 cha chai(option)

Limao/ndimu 2

 


Jinsi ya kupika.

Osha kuku wako vizuri,weka spice zote na limao au ndimu. Wacha vichanganyike kwa nusu saa.

Chukua tray yako kubwa (Kama ile ya kuchomea cake)weka kuku wako humu oka kwa dk thelathini kakikisha hakauki.


Jinsi ya kupika wali

Kaanga vitunguu vyako Kama vile vya biriani viweke pembeni.

Roweka mchele wako kwa dk 15

Weka katika sufuria maji mag 3bandika jikoni yakichemka weka mchele na chumvi uangalie usishikane,na usiive sana(uchemshe kwa dk 5)


Toa kuku wako Ktk oven chukua wali wako kidogo weka juu yake halafu weka vitunguu   na korianda,weka soya souse ,malizia wali uliobakia halafu nyunyizia soya souse yako juu ya wali.

Oka tena kwa dk 10 toa tayari kwa kuliwa.


0 comments:

Post a Comment

Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!