Sunday 19 June 2016

Thanks to my brodaz in law for the  dinner date I real appreciate.
The food  was very yummy yummy

Tuesday 7 June 2016

Kutokana na familia yangu kuepuka sana Kula Mafuta hivyo vyakula vyetu vingi ninaepuka kutumia mafuta mengi wakati wa kupika au kutoweka Kabisa.
Hivyo nimeamua kutwist recipe ya  Shruba nimeamua kufanya chukuchuku.
Usijali  nitaweka inayotumia mafuta.

Mahitaji
Oats / ngano  nusu kikombe
Nyama (mbavu) nusu kilo
Nyanya fresh moja
Kitunguu maji kimoja kikubwa
Kitunguu swaumu kijiko cha chakula1
Pilipili manga kijiko cha chai 1
Chumvi nusu kijiko cha chai
Viungo vya pilau  kijiko cha chakula1
Unga wa ngano kijiko kimoja cha chakula
Korianda

Jinsi ya Kupika

Chemsha oats/ngano  weka pembeni
Osha nyama yako weka katika sufuria chemsha ikiiva iache na supu
Saga viungo vyote pamoja weka
mimina katika nyama,weka viungo vya pilau,mag,pilipili manga,wacha vichemke kwa pamoja kwa dakika tano halafu weka ngano funika wacha ichemke wa nusu saa.
Weka unga wa ngano katika kibakuli n.a. maji mimina katika shruba  wacha uchemke kwa dakika 10.
Epua tayari kwa kuliwa..
NB:Wakati wa kunywa waweza weka siki au ndimu upendavyo

Tuesday 19 April 2016


Imeandikwa na Dk. Boaz Mkumbo

MOJA ya vyakula ambavyo tumekuwa tukitumia kwa wingi hasa Watanzania wenye kipato cha kati na chini kabisa ni vyakula vya aina kuu tatu, Wanga, Protini na Mafuta (Fats).

Na kwa kiwango kidogo sana tunatumia vitamin na madini katika milo yetu. Moja ya masomo ya chakula tunayofundishwa ni kula mlo kamili.Watu wengi tumekuwa tukitumia elimu hiyo hadi hapa tulipofika.

Napenda kusema tu kwamba mlo kamili ni kwa ajili ya mtu mzima ambaye hana ugonjwa wowote na ni kwa yule tu ambaye hataki kula kiafya.

Napenda kusema haya kwa sababu tumekuwa tukila vyakula vya namna ile ile lakini tumekuwa tukiugua mno magonjwa mbalimbali yatokanayo na lishe mbovu. Hadi sasa ugonjwa wa kisukari hapa duniani unaua zaidi ya ugonjwa wa UKIMWI, swali la kujiuliza je, tumejitenga wapi mbali katika lishe?

Leo nataka nikueleze kidogo kuhusu sayansi ya chakula aina ya wanga. Maana kila mtu ninayemwelekeza njia sahihi ya kupunguza uzito anakwambia nitaishije bila chakula cha wanga? Mwili wako hutumia vyakula vikuu aina tatu ambavyo ni wanga, protini na mafuta.

Na unatakiwa ujue kuwa gramu moja ya wanga hutengeneza nishati ya mwili kalori nne, ambapo protini nayo hutengeneza kalori nne na Fats hutengeneza kalori tisa. Unaona ni zaidi ya mara mbili ya nishati zinazotengenezwa na chakula cha wanga.

Hii ina maana kuwa ninaposema kuwa tunaweza kupunguza wanga na ukaishi ukiwa na nguvu nyingi zaidi hata ya ulivyo kuwa katika lishe ya wanga nyingi.

KWA NINI NAKUSHAURI UPUNGUZE WANGA KIAFYA?

Unapokuwa umepunguza wanga au kuacha kabisa ulaji wa vyakula vyenye wanga nyingi, mfano mikate, ugali, wali na tambi. Hakikisha kitendo hicho kiendane na kuongeza kiwango cha mafuta na vyakula vya protini mwilini mwako katika lishe yako. Hii itaufanya mwili wako kuanza kutumia mafuta kama nishati ya mwili ya kwanza kujitengenezea nguvu.

Viungo vya binadamu kama ini na figo vinapokuwa vinatumia mafuta kuzalisha nishati ya mwili hutengeneza viini vya nishati viitwavyo Ketone Bodies, ambavyo hivi ndivyo hutumiwa na seli za mwili kujitengenezea nishati kwa wingi.

Hivyo basi, unapokuwa unajizuia kutumia vyakula vya wanga mwili wako utatumia karibia siku tano hadi wiki kuanza kutumia mafuta kama nishati ya mwili na hicho kitendo tunaita Keto Adaption.

Ningependa kusema kwamba Keto Adaption ni ile hali ya mwili wako kujenga mazoea ya kutumia mafuta kama chanzo cha nishati ya mwili na hapo ndipo utaanza kuona mabadiliko katika mwili wako makubwa.

Utakuwa unajisikia mwenye nguvu na unatashangaaa dalili mbalimbali zilizokuwa zinakusumbua zinapotea hii ni kwa sababu ya uwezo mkubwa wa ketone bodies katika mwili wako dhidi ya glucose.

Sote tunajua kwamba ulaji wa vyakula vya wanga kwa wingi na vyakula vyenye sukari nyingi vinaongeza kiwango cha sukari kwenye damu zaidi ya kiwango ambacho mwili wako unaweza kuhimili.

Mfano; kiwango cha kawaida cha sukari kinachohitajika mwilini mwako ni kijiko kimoja cha chai, hiki ni kiwango ambacho hakiwezi kukuletea matatizo. Basi kama binadamu anaishi kwa sukari inayokadiriwa kuwapo kwenye damu kama kijiko kimoja tu cha chai.

Unywaji wa soda moja unaweza kuongeza zaidi ya vijiko 10, hivyo basi mwili wako unakuwa unashindwa kuhimili sukari iliyozidi.

Kwa wale wanaopenda kula baga, inakadiliwa kuwa baga moja ya kati inaweza kutoa sukari zaidi ya vijiko 16 kwenye damu.

Swali la kujiuliza mwili unapeleka wapi sukari iliyozidi wakati miili yetu inahitaji sukari kiwango kidogo kama kijiko kimoja tu kuishi?
Mwili hutengeneza maji kutoka kwenye seli za kongosho ziitwazo beta seli, maji haya ni homon iitwayo Insulin, kazi kubwa ya insulin ni kutunza glucose hii katika damu kwa matumizi ya baadae, na inatunza katika kiasi maalumu katika mfumo wa Glycogen na kiasi kikubwa katika mafuta.

Hivyo basi, mafuta haya huhifadhiwa katika sehemu mbalimbali kama tumboni, shingoni, mikononi, kifuani na kiunoni. Mafuta haya huhifadhiwa katika mfumo wa Tryglycerides ambayo haya ni miongoni ya mafuta mabaya mwilini mwako.

Sasa mtu anayekwambia wanga nyingi katika chakula chako ni salama anakudanganya kwa kiasi kikubwa kwani tunaona jinsi gani ulaji wa kiwango kingi cha vyakula vya wanga na sukari vinavyosababisha sukari kupanda kupita kiasi na insulin kuanza kuhifadhi katika mafuta.

Kila siku nasema, tumekaririshwa adui mkuu ni fats na kujisahau ulaji mbovu wa vyakula vya wanga huku tukiishia kulea vitambi na magonjwa sugu, hii yote ni kutokuwa na ufuatiliaji wa lishe nzuri na salama kwako.

MADHARA MENGINE YA SUKARI

Napenda kuwarudisha nyuma kidogo katika somo la bailojia. Tulijifunza kuwa miili yetu imejengwa kwa kiini kidogo sana kiitwacho seli ambapo shughuli zote za mwili zinafanyika humo.

Nilijifunza kuwa ndani ya seli kuna viungo vidogo vidogo navifananisha na (Apartments kwenye nyumba kubwa) moja wapo ni Mitochondria, hiki ni kiungo kidogo katika seli ambacho kinahusika na kuzalisha nishati ya mwili tu. Pia nikikumbuka watu wote tulijifunza kwamba mwili wetu hujitenegenezea nishati ya mwili au nguvu kupitia kuifanyia kazi sukari iliyo ndani ya damu baada ya kuingia ndani ya seli.

Hivyo basi insulin ni kama ufunguo ambao unafungua milango ili sukari iweze kuingia ndani ya seli hadi kwenye mitochondria. Mwili wako unapokuwa unatumia hewa ya oxygen kuna uwezekano mkubwa wa kupatikana kwa athari iitwayo Oxdative stress.

Hii ndiyo inayofanya chuma kipate kutu, hii ndiyo inayofanya mafuta ukiyaweka kwenye jua kwa muda mrefu yanaharibika. Basi mwili wako unakuwa unatengeneza vihatarishi viitwavyo Reactive Oxygen Species kwa kifupi huitwa Free Radicals.

Hizi ni sumu ambazo hupatikana wakati mwili unajitenegenezea nishati yake kwa kutumia oxygen na hizi zinapokuwa kiwango kikubwa huweza kuharibu kabisa seli na kuziua na pia zinaweza kupelekea kupata magonjwa sugu kama saratani.

Hivyo, tafiti zinaonesha kwamba vyakula vya wanga na sukari vina matokeo makubwa ya kutenegeneza Free Radicals nyingi kupita kiasi.

Miili yetu ina kiwango fulani cha viondoa sumu ambavyo vinaipunguza sumu ya free radicals kuepusha kusababisha magonjwa kwa kuziua seli.

Lakini panapokuwa na kiwango kikubwa cha uzalishaji wa free radicals mwili unashindwa kuhimili na hatimaye free radicals zinaanza kuleta madhara mwilini mwako. Kadri mitochondria zinavyodhoofika ndivyo magonjwa nyemelezi ya lishe yanavyotukabili kila kukicha.

Thursday 18 February 2016

Mahitaji
Unga wa ngano 250g
Butter 250g
Mayai 9
Baking powder kijiko cha chai1
kuku wa kusaga 2cups
Chumvi kijiko cha chai 1
Sukari 1/3cup
Kungu manga 1/2 kijiko cha chai(sio lazima)
Mdalasini kijiko cha chai 1
Curry powder kijiko cha chai 1
Kitunguu swaumu kijiko cha chai 1
Tangawizi kijiko cha chai 1
Chicken stock kijiko 1/2 cha chai
Pilipili mtama 1/2 kijiko cha chai
Ndimu/limau moja
Pilipili hoho 1/2 kila rangi

Jinsi ya kupika
Muoshe kuku wako vizuri as iwe na ngozi muweke viungo vyote mbandike jikoni isipokuwa usiweke pilipili hoho.
Mwache achemke na hayo Maji yakikauka muweke pembeni apoe.
Kama utakuwa haujapata kuku wa kusaga umechemsha kuku mzima basi akipoa mnyambue nyambue au msage katika blender,muweke pembeni.
Saga siagi na sukari pamoja na mayai 3,yakichanganyika weka unga na baking powder.
Ikichanganyika vizuri weka katika chombo cha kuchomea,chukua kuku wako  changanya na mayai 3 mimina juu ya ule unga wako wa keki uliopo katika chombo cha kuchomea,halafu piga Yale mayai matatu yaliyobakia ya changanye na pilipili hoho miminia juu.
Weka katika oven moto 350.

Tuesday 16 February 2016


Mahitaji

Mchele mag 2
Yai moja
Nazi kikopo kimoja
Hamira kijiko kimoja cha chakula mfuto
Sukari nusu mag
Baking powder pinch mbili
Maziwa ya maji yawe sawa na nazi.
Iliki kijiko cha chai kimoja.
unga wa ngano kijiko kimoja cha chakula.

Jinsi  ya kupika.
Roweka mchele  hadi ulainike.
Weka katika  blender kila kitu kasoro unga wa ngano,  saga hadi  ulainike weka unga wa ngano saga kidogo mimina katika bakuli wacha kwa lisaa moja uumuke.
Choma vitumbua vyako,usivinyime mafutaa.

NB:unga wa ngano unasaidia kufanya kitumbua crunch

Saturday 30 January 2016

Mahitaji:-
Viazi mbatata kg 1
Cornflour(starch) vijiko 2 chakula 
Siagi vjk 2 chakula
Chumvi kijiko1 chai
Tomato ketchup vijiko 3 chakula
Tomato puree kijiko 1 chakula
Tandoor masala powder 1/2 kjk chai
Kitunguu saumu kilichosagwa 1/4 kijiko chai
Pili pili ya unga (red chili powder) 1/4 kijiko chai
Binzari ya unga( cumin powder) 1/4 kijiko chai
Manjano (turmeric) 1/8 kijikocchai
Pilipili ya kijani ilokatwa katwa ( green chilli) 1
Limao kipande
Mafuta ya kukaangia
Mkono mmoja kotmir kupambia (for garnish)

MAELEKEZO:-
1.Tia mafuta ktk frying pan au sufuria jikoni , moto uwe wa kati (mediuh heat). Kaanga chips zako

2.Epua acha zichuje mafuta katika paper towels kisha utazikaanga tena kwa mara ya pili zikauke zadi

3. Katika sufuria jikoni pasha moto siagi iyeyuke,toa sufuria jikoni kisha tia cornflour,pamoja na mahitaji yote isipokuwa limao na kotmir.

4 Rudisha sufuria jikoni na kisha changanya vitu vyote ukikoroga hadi mchanganyiko uwe mzito.

5 Punguza moto kisha tia chips zako na geuza zienee viungo vizuri

6 Epua kisha kamulia limao na nyunyiza kotmir ulizokata kata juu. Masala chips tayari kwa kula.

Kijiko cha chai (teaspoon)
Kijiko cha chakula (Tablespoon)

Thursday 14 January 2016

Kuwa na harufu mbaya mdomoni ni kitendo kinachoweza kuathiri maisha ya mtu kimahusiano si kwa mpenzi tu bali marafiki na jamii kwa ujumla. Pia kuwa na harufu mbaya mdomoni uondoa haiba ya kupendwa kwani hata unapoongea wengi watakwepa kuongea moja kwa moja na wewe kwa sababu ya harufu mbaya inayotoka mdomoni mwako.

Chakula unachokula kina athiri hewa inayotoka mdomoni au sehemu nyingine za mwili wako. Baadhi ya vyakula vina matokeo mabaya sana kwa hurufu unayotoa mdomoni. Harufu mbaya mdomoni si ugonjwa wa kuambukiza haina haja kuogopa ukikutana na mtu mwenye harufu mbaya mdomoni kwamba atakuambukiza.

Pia tatizo kubwa ni kwamba watu wenye harufu mbaya mdomoni hawajijui kwamba wana harufu mbaya. Asilimia 85 - 90% ya tatizo la harufu mbaya mdomoni asili yake ni kinywa chenyewe. Pia kiwango cha harufu hutofautiana kutokana na muda (mchana, usiku na asubuhi).

Harufu nyingi mbaya mdomoni hutokana na vyakula vyenye asilia ya protein. Kuna zaidi ya aina 600 ya bacteria wanaoishi kwenye kinywa cha Binadamu (sehemu ya juu ya ulimi, fizi na kuzunguka meno).

KINACHO SABABISHA HARUFU MBAYA MDOMONI

Kutokuwa makini na usafi wa kinywa kama vile kupiga mswaki vizuri kunakoacha mabaki ya chakula ambayo huoza na kusababisha harufu mbaya mdomoni. (Wengi hupiga mswaki haraka haraka na kuacha mabaki ya chakula). Maambukizi ya magonjwa kama vile fizi kutoka damu, mfumo wa upumuaji na kisukari. Kinywa kuwa kikavu kutokana na madawa (medications) Kuvuta sigara, kunywa kahawa, ulaji wa vyakula vyenye viungo vikali kama vile vitunguu maji au thaumu.

NAMNA YA KUJUA KAMA UNA HARUFU MBAYA MDOMONI

Wanasayansi wamekiri kwamba ni ngumu sana mtu kujijua mwenyewe kama ana harufu mbaya kwa sababu ya mazoea (habituation).
Ni rahisi sana kutambua harufu kutoka kwenye kinywa cha mtu mwingine. Unaweza kutambua kama una harufu mbaya mdomoni kwa kumuuliza mtu unayemuamini.
Pia unaweza kujua harufu mbaya kwa kulamba nyuma ya kiganja na kunusa, wengine hupumua mbele ya kioo na kunusa. Pia unaweza kutumia kijiti cha kuchokonolea meno na kukinusa. Kisayansi unaweza kutumia vifaa kama Halimeter, Gas Chromatography na BANA Test.

NAMNA YA KUJILINDA NA HARUFU MBAYA MDOMONI (TIBA) 

Kula vyakula vyenye afya na vyakula ambavyo wakati unakula vinaweza kusafisha kinywa vizuri. Kusafisha meno mara kwa mara au kwa uchache mara mbili kwa siku asubuhi na baada ya mlo wa usiku, hii usaidia kuondoa au kujikinga na harufu mbaya mdomoni. Vilevile unashauriwa kutumia KISAFISHA ULIMI (tongue cleaner) kusafishia ulimi wako. Tumia bazooka (chewing gum) ambazo husaidia kuongeza kiasi cha mate kwenye kimywa kilichokauka. Baadhi ya gums zina viungo vinavyoondoa harufu mbaya mdomoni na zingine husafisha kinywa na bacteria wanaosababisha harufu mbaya. Tumia dawa ya kusukutua mdomoni (mouthwash) kabla ya kulala usiku. Kuwa makini na afya ya kichwa chako kama vile kupiga mswaki vizuri, kuondoa mabaki ya vyakula kwenye meno na kumuona daktari kila unapoona una Matatizo ya meno au kinywa au kila baada ya miezi sita kwa uchache.
Kuhakikisha unakunywa maji ya kutosha kila siku angalau glass mbili za maji.
Mwone daktari wako ukiona una tatizo la harufu mbaya mdomoni.

NAMNA YA KUJIKINGA NA KUONDOA HARUFU MBAYA MDOMONI!

Watu wengi husumbuliwa na tatizo la kunuka mdomo bila hata kujijua hivyo kuwa kero kwa wenzao na wakati mwingine hujishushia hadhi mbele ya jamii. Mara nyingi ugonjwa wa kunuka mdomo (Halitosis) husababishwa na uchafu wa kinywa na ulaji wa vyakula usiosahihi lakini ni tatizo linalotibika.

Ni rahisi kulizuia na kuliondoa tatizo la kunuka mdomo iwapo utaamua kufuata kanuni za usafi wa kinywa na unywaji wa maji kwa kufuata kwa makini muongozo ufuatao:

KUPIGA MSWAKI

Kitu cha kwanza kufanya ni kupiga mswaki kwa ukamilifu kila uamkapo asubuhi. Wakati wa kupiga mswaki, utatakiwa siyo tu kusugua meno, bali pia ulimi, sehemu ya katikati hadi karibu na koromeo kwa kusugua vizuri. 
Vile vile kila uamkapo baada ya kulala mchana au jioni, hakikisha unapiga mswaki, kwani bakteria wa kinywani, hutawala kinywa kila ulalapo. Mara baada ya kupiga mswaki na kusugua ulimi sawaswa, hakikisha unasukutua vizuri kwa maji, kwani hapa ndipo baadhi ya watu hukosea kwa kupiga mswaki bila kusukutua kwa maji.

KUNYWA MAJI MENGI

Maji ni muhimu sana karibu kila eneo la mwili wa binadamu. Unywaji wa maji ya kutosha kila siku utakusaidia kudhibiti na hatimaye kuondoa tatizo la kunuka mdomo. Unywaji wa maji mengi ni muhimu, hasa kwa wale watu wenye ugonjwa wa kukauka midomo (xerostomia).

Mara nyingi harufu itokayo mdomoni, hutokea tumboni na siyo kinywaji peke yake kama unavyoweza kudhani. Hivyo, kama tumbo litakuwa chafu, hata kama utasafisha kinywa vizuri bado harufu mbaya inaweza kuendelea kutoka. Harufu mbaya ya tumboni hutokea pale tumbo linapokuwa chafu kutokana na kutopata choo kwa muda mrefu. Miongoni mwa mambo yanayochangia kukosekana kwa choo kwa muda mrefu ni pamoja na tabia ya kutokunywa maji ya kutosha kwa siku, hivyo hakikisha unakunywa maji, kiasi kisichopungua lita moja na nusu hadi mbili au zaidi, kutegemeana na kazi unazozifanya.

Ukiwa na tatizo la kukaukiwa maji mwilini kila mara, mwili hujaribu kutumia njia zake za kiasili kupunguza uzalishaji wa mate ili kuhifadhi maji kwa ajiili ya matumizi mengine, kitendo hicho huchangia kunukisha mdomo kwa sababu ndani ya mate huwa kuna kinga muhimu dhidi ya baktetria wanaonukisha kinywa.

Kwa upande mwingine, ili kuzuia kinywa kunuka pale mdomo unapokuwa umekaukiwa na mate, ni vizuri kutafuna vitu kama bazooka (chewing gum) yoyote ili kuzalisha mate ambayo huhitajika katika kudhibiti bakteria.

MWISHO:

Hakikisha unasukutua sawaswa baada ya kula chakula chochote, hata kama ni juisi isipokuwa unapokunywa maji tu ya kawaida. Bila shaka, ukizingatia haya, tatizo ulilonalo la kunuka mdomo litataoweka na kubaki historia.


Saturday 9 January 2016

Mahitaji

Ndizi Tamu 5
Kikopo kimoja cha Nazi
Chimvi pinch Mbili
Sukari kijiko cha chakula kimono
Iliki kijiko cha chai kimoja
Custard powder kijiko cha chai kimoja
Maziwa wa unga kijiko cha chakula kimoja
Maji  mag moja

Jinsi ya kupika
Katakakata ndizi zako,ndizi moja toa vipande vinne panga katika sufuria,weka  chumvi,sukari,iliki,mimina maji bandika bikini funika maji yakiukia weka nazi yako wacha ichemke usinifike,wacha kwa dk 3,chukua maziwa yako ya unga (nimetumia nido) weka katika kikombe,weka custard powder changanya na maji moto robo kikombe hakikisha vimelainika mimina katika ndizi wacha kwa dakika 3  epua ndizi zako tayari,
Chakula hiki ni  kwa ajili ya watu watatu.
Unaweza kutumia kwa chai,uji wa Dona,sembe,bada/unga wa muhogo.
Nb: ndizi zisiwe zimeiva sanaaa kuepuka kuhorojeka wakati wa kupika.
Enjoy pishi lako.

Sunday 6 September 2015



Mahitaji

Mchele 2 cups(inategemea na familia yako)

Chumvi nusu kijiko cha chai

Korianda vijiko vitatu vya vyakula(majani)

Soya souse vijiko viwili vya chakula

Vitunguu maji vikubwa vitano.



Kitoweo

Kuku 1/nyama kilo moja

Mahitaji

Kitunguu swaumu kijiko cha chakula kimoja

Tangawizi kijiko cha chakula 1

Paprika kijiko cha chakula 1

Pilipili mtama 1kijiko cha chai

Pilipili mbuzi iliyosagwa 1/2 cha chai(option)

Limao/ndimu 2

 


Jinsi ya kupika.

Osha kuku wako vizuri,weka spice zote na limao au ndimu. Wacha vichanganyike kwa nusu saa.

Chukua tray yako kubwa (Kama ile ya kuchomea cake)weka kuku wako humu oka kwa dk thelathini kakikisha hakauki.


Jinsi ya kupika wali

Kaanga vitunguu vyako Kama vile vya biriani viweke pembeni.

Roweka mchele wako kwa dk 15

Weka katika sufuria maji mag 3bandika jikoni yakichemka weka mchele na chumvi uangalie usishikane,na usiive sana(uchemshe kwa dk 5)


Toa kuku wako Ktk oven chukua wali wako kidogo weka juu yake halafu weka vitunguu   na korianda,weka soya souse ,malizia wali uliobakia halafu nyunyizia soya souse yako juu ya wali.

Oka tena kwa dk 10 toa tayari kwa kuliwa.


Wednesday 22 July 2015

Mafua ni ugonjwa unaosumbua watu kila mwaka, hasa yanapoanza kutokea mabadiliko ya hali ya hewa, kutoka msimu wa joto kuingia baridi au kutoka msimu wa kiangazi kuingiza masika. Ili kujikinga na ugonjwa wa mafua, ni lazima mwili uwe na kinga ya kutosha.

Orodha ya vyakula vifuatavyo vimeelezwa kuwa na uwezo mkubwa wa kuimarisha kinga ya mwili na kupambana na maambukizi mengine kwa kuwa na kiasi kikubwa cha protini na virutubisho vingine.

SUPU YA KUKU
Supu ya kuku wa kienyeji inaelezwa kuwa na virutubisho vinavyosaidia kupunguza utokaji wa makamasi. Utapata virutubisho vingi zaidi ukitengeneza supu ya kuku kwa kuchanganya na mboga za majani. Weka chumvi kiasi kidogo katika supu hiyo.

VITUNGUU SAUMU
Vitunguu saumu vina kirutubisho aina ya ‘allicin’ ambacho kina uwezo wa kutoa kinga dhidi ya magonjwa mbalimbali ya kuambukiza. Kitunguu saumu kinatoa kinga halikadhalika kinapunguza muda wa mtu kuumwa na mafua. Tumia kitunguu hicho kwa kupika kwenye chakula au kwa kutafuna punje zake.

CHAI
Chai, hasa ya kijani, (green tea) ina virutubisho vya kuimarisha kinga ya mwili. Utafiti wa hivi karibuni uliofanywa na jarida moja la masuala ya virutubisho nchini Marekani (Journal of the American College of Nutrition) umeonesha kuwa watu wanaotumia chai kwa mpangilio maalum hawasumbuliwi mara kwa mara na mafua pamoja na magonjwa mengine ya kuambukiza, huwa salama na mafua au siku za kuumwa mafua hupungua kwa asilimia 36 ukilinganisha na wale wasiokuwa na kinga imara.

Hata hivyo, tahadhari inatolewa kwa watoto wa shule kutokupewa kiasi kingi cha chai kwa siku. Unywaji wa kikombe kimoja kwa siku kwa mtoto wa shule siyo mbaya. Kwa mtu mzima, asizidishe vikombe vitatu kwa siku. Ikumbukwe kuwa chai inapotumika kwa wingi kupita kiasi, huweza kusababisha pia tatizo la kukosa choo kwa muda mrefu. Kunywa kiasi kwa afya yako.

MACHUNGWA, PILIPILI KALI
Utafiti unaonesha kwamba ulaji wa vyakula vyenye Vitamin C kwa wingi kila siku husaidia kuondoa au kuzuia ugonjwa wa mafua. Miongoni mwa vyakula vyenye kiwango kikubwa cha Vitamin C ni pamoja na machungwa, mboga za majani aina ya Brokoli na pilipili kali.
Ili kupata kiasi kingi cha Vitamin C, inashauriwa machungwa yaliwe pamoja na nyama zake za ndani au kunywa juisi yake.

ASALI
Kama inavyojulikana, asali ni tiba ya matatizo mengi ya kiafya, miongoni mwa hayo ni pamoja na mafua. Asali inasaida kuondoa kikohozi na muwasho kwenye koo. Halikadhalika, asali inaweza kutumiwa na watoto wadogo kama dawa.

Watoto wanaoruhusiwa kutumia asali kama tiba ni wa umri kati ya miaka 2 hadi 5. Hawa dozi yao ni nusu kijiko kidogo cha asali, wenye umri wa miaka 6-11 wapewe kijiko kimoja kidogo na wenye umri kuanzia miaka 12 hadi 18, wapewe vijiko vidogo viwili vya asali wakati wa kulala.

MTINDI
Kutokana na kiwango kikubwa cha protini ilichonacho, Mtindi ni chakula kingine kinachofaa kuliwa na mtu mwenye mafua ili kupunduza siku za kusumbuliwa na ugonjwa kukohoa.

CHOKOLETI NYEUSI
Wataalamu wanakubaliana kuwa ulaji wa ‘chocolate’ nyeusi (dark chocolate) huimarisha kinga ya mwili, hivyo inapoliwa na mgonjwa wa mafua huweza kumpa ahueni mgonjwa kwa namna moja ama nyingine. Halikadhalika huwa kinga kwa maambukizi mengine.

PWEZA
Samaki aina ya pweza wana virutubisho vingi vya kuongeza kinga ya mwili yenye uwezo wa kupambana na bakteria pamoja na virusi vya mafua. Kiasi kidogo cha pweza, awe wa kukaangwa au kuchemshwa kama supu, anafaa kuliwa mara kwa mara kuimarisha kinga ya mwili.

VIAZI VITAMU
Kirutubisho aina ya ‘Beta-carotene’ huimarisha kinga ya mwili. Kirutubisho hicho huwa ni muhimu kwa ustawi na uimarishaji wa kinga mwilini na kinapatikana kwa wingi kwenye viazi vitamu na vyakula vingine kama vile karoti, maboga na mayai, (kiini).

Kwa ujumla, suala la kuimarisha kinga ya mwili ni muhimu kwa afya zetu. Ulaji wa vyakula vilivyotajwa hapo juu na vingine, unatakiwa kuwa ni wa mara kwa mara kama siyo wa kudumu, kwa sababu mwili unapokosa kinga imara, ni rahisi kushambuliwa na maradhi ya kuambukiza.
Subscribe to RSS Feed Follow me on Twitter!